Posts

Showing posts with the label Mapishi

JINSI YA KUPIKA MAANDAZI

Image
JINSI YA KUPIKA MAANDAZI LAINI. MAHITAJI YA MAANDAZI 1. Unga - 5 Vikombe. 2. Tui la Nazi zito vugu vugu - 1 ¼ kikombe. 3. Sukari - 3/4 kikombe cha chai. 4. Samli iliyoyayushwa au mafuta - 3 vijiko vya Supu. 5.Hamirah - 2 Vijiko vya Supu. 6. Hiliki - 1/2 Kijiko cha chai. 7. Mafuta ya kukaangia. NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA. 1. Ndani ya kibakuli kidogo, mimina hamira na na vijiko viwili vya kulia vya tui. Weka kando mpaka hamira ianze kufura, kama dakika 5-10. 2. Pasha samli moto: 3. Ndani ya bakuli kubwa au sinia, changanya unga, sukari, iliki na samli ikiwa bado moto moto. 4. Mimina hamira ndani ya mchanganyiko wa unga. 5. Changanya na ukande huku ukitumia lile tui la nazi. Tui likipungua unaweza ukaongeza maziwa. 6. Kanda unga mpaka uwe laini. 7. Kata madonge *12 au 15 uyaweke kwenye baraza iliyonyunyiziwa unga na uyafunike ili yapate kufura na yasikauke. *Ukipenda maandazi manene fanya madonge 12. Ukipenda mepesi fanya madonge 15. 8. Madonge yakifura,

JINSI YA KUPIKA DAGAA WATAMU ZAIDI

Image
🥕🧅Jifunze Jinsi Ya Kupika roast la Dagaa mwanza Watamu 🥕🧅 🥕🧅 MAHITAJI 🥕🧅 1️⃣ Dagaa 2️⃣ Limao 3️⃣ Karoti 4️⃣ Bamia 5️⃣ Kituunguu Maji 6️⃣ Kitunguu Thoum 7️⃣ Pilipili Mbuzi 8️⃣ Pilipili Manga 9️⃣ Pilipili Boga 1️⃣0️⃣ Nyanya Maji 1️⃣1️⃣ Tomato Paste 🥕🧅 NAMNA 🥕🧅 1️⃣ Toa Vichwa Dagaa Wako 2️⃣ Chemsha Maji Yakichemka Yaipue 3️⃣ Weka Dagaa Kwenye Maji Ya Moto Kwa Dk20 Ili Uchafu Na Mawe Vitoweke 4️⃣ Waoshe Dagaa Vile Wewe Unataka Kama Na Sabuni, Maji Mara8 Ili Mradi Wawe Salama Kwa Utafunaji 5️⃣ Waweke Kwenye Nyungo/ungo Watawanye Waweke Juani Ili Wakauke Kupunguza Matumizi Ya Mafuta Kipindi Unawakaanga 6️⃣ Kipindi Dagaa Wapo Juani Andaa Viungo Vyako Kwa Usafi Na Kuvikata Kwa Mikato Upendayo 🔛 Bamia 🔛 Karoti 🔛 Pilipili Boga 🔛 Pilipili Manga 🔛 Kitunguu Maji 🔛 Kitunguu Thoum 7️⃣ Weka Sufuria Jikoni Tia Mafuta Ya Kula Weka Na Chumvi Kiasi Yakipata Moto Weka Dagaa Zako Kaanga, Wakianza Kuwa Na Rangi Ya Udhur

JINSI YA KUPIKA MAKANGE YA SAMAKI

Image
Kaributena katika blog yangu uko na International Admin leo naenda kukuletea pishi la Makange ya samaki. Makange ni kati ya mboga rahisi sana kupika na utashangaa kujua kuwa huenda ulikuwa unajichelewesha kuandaa mboga hiyo nyumbani kwako kwa kuogopa vile unayakuta katika hoteli kubwa nyingi na yanavyowekwa kwenye sahani. Huenda umetamani kupika mboga ya makange kwa muda mrefu lakini ukadhani kwa namna ulivyowahi kuiona kwenye sahani, siyo mboga rahisi kupika. TUANZE MAHITAJI ✓ Kitunguu kimoja ✓ Nyanya kubwa 3 ✓ Karoti moja ✓ Hoho moja ✓ Ndimu moja ✓Kitunguu saumu na tangawizi iliyosagwa kijiko kimoja (vyote kwa pamoja) ✓ Tomato fresh 2 ✓ Chumvi kiasi ✓ Binzari nyembamba na pilipili manga ya unga kijiko kimoja cha chakula ✓ Curry powder kijiko kimoja cha chakula ✓ Binzari ya mchuzi kijiko kimoja cha chai ✓ Soya sauce ya kukoza vijiko 3 vya chakula ✓ Maji robo kikombe ✓ Mafuta ya kupikia vijiko 3-4 ✓ Spice ya samaki kijiko 1 Cha chakula ✓ Samaki mkubwa mmo

JINSI YA KUTENGENEZA MANGO PICKLE (CHACHANDU YA EMBE) NYUMBANI

Image
Karibu tena katika darasa letu la mapishi basi leo naenda kukuletea namna ya kuandaa achari ya embe nyumbani unaweza kula kwa ugali au chochote ukipendacho. MAHITAJI. ✓Maembe mabichi (usitumie embe zilizoiva au zilizoanza kuiva) ✓ Pilipili mbichi (kama ukipenda) ✓ Achari masala ✓Masala ya kuwasha ✓ Mafuta ya kupikia ✓ Binzari ya njano (tumeric powder) ✓ Chumvi kiasi. MATAYARISHO. ✓ Osha vizuri embe zako na uzikate Kate saizi uipendayo lakini usimenye maganga (Kata vikonyo cha juu na chini) ✓ Loweka embe zako weka na chumvi kwa muda wa siku mbili au tatu Kisha utazianika kwa siku moja au mbili. (Angalia zisikauke Sana zitaleta ugumu wakati wa kula) ✓ Weka mafuta jikoni mpaka yapate moto Kisha yatoe yaweke pembeni yapoe yawe Kama ulivyoyatoa dukani. ✓Chukua chombo chenye nafasi ya kutosha changanya vitu vyote pamoja na mafuta mpaka vichanganyike vizuri ✓ Kisha anika mchanganyiko wako kwa siku kadhaa ili uive vizuri na hapo utakuwa tayari kwa matumizi

JINSI YA KUPIKA BIRIANI TAMU YA KUKU

Image
Kaributena katika darasa letu la mapishi basi leo naenda kukuletea namna ya kuandaa biriani nzuri ya kuku. MAHITAJI kuku 1kg Mchele wa basmati/ wakawaida (Hapa nitatumia nusu) Vitunguu maji 1/4 Nyanya zilizosagwa tano Nyanya ya mkebe Vitunguu saumu punje 10 Pilipili za kijani 4 Mafuta 1/4 Mdalasini vijiti 5 Hiliki punje 10 Tangawizi vijiko 2 vya chakula Majani ya nanaa yaliyokatwa kibakuli kidogo 1 Binzari nyembamba kijiko 1 cha chai Chumvi kijiko 1 cha chai Manjano 1/2 kijiko cha chai Zafarani 1/2 kijiko cha chai Kotmiri iliyokatwa 1/4 kikombe Maziwa ya mtindi kikombe 1 Njegere (ukipenda) JINSI YA KUANDAA Loweka mchele w kwa dakika 15 hadi 30 Weka mafuta kwenye sifuria, yakishapata moto kaanga vitunguu maji hadi viwe na rangi ya brown kisha chota vitunguu robotatu ya ulivyovikaangaweka pembeni vingine vibaki kwenye sufuria. Twanga kwa pamoja binzari nyembamba, kitunguu swaumu, tangawizi, nusu ya pilipili na vijiti vya mdalasini, kisha weka robo tatu ya vit

PILAU TAMU YA NYAMA.

Image
NAFASI ZA SENSA 2022 www.tamisemi.go.tz JIANDAE KUHESABIWA Karibu tena, basi leo International Admin anakuletea namna ya kupika pilau tamu ya nyama. Usiondoke angalia mwanzo mwisho, enjoy! MAHITAJI ✓ Mchele (unaweza kuwa basmati au wakawaida) ✓ Nyama (mbuzi au ng'ombe) ✓ Viazi mbatata kiasi ✓ Unga wa pilau (nimeelekeza katika post ya nyuma hapo namna ya kuandaa) ✓ Chumvi kiasi ✓ Mafuta kiasi ✓ Vitunguu maji vitatu kitunguu swaum kilichopondwa ✓Binzari nyembamba (uzile) uloweke kwenye maji kidogo. . NAMNA YA KUPIKA 1. Chemsha nyama yako mpaka iive itie na chumvi kiasi (Supu iweke pembeni) 2. Kaanga viazi mbatata na viive (visiwe brown) Kisha vitoe vikiwa bado na rangi nyeupe. (Wengine hawakaangi, ila ukikaanga mbatata zako zitakuwa na ladha nzuri zaidi) 3. Kaanga vitunguu maji mpaka viwe brown (angalia visiungue vitabadili ladha ya chakula) 4. Weka mdalasini kaanga pamoja, Kisha weka uzile na hiliki na unga wa pilau kidogo Kish

JINSI YA KUANDAA VIUNGO VYA PILAU VYENYE HARUFU NZURI.

Image
NAFASI ZA SENSA 2022 www.tamisemi.go.tz JIANDAE KUHESABIWA Karibu kwa mara nyingine ukiwa na International Admin leo nitaenda kukuonesha namna ya kuandaa viungo vya pilau vyenye harufu. Ni rahisi sana, enjoy! MAHITAJI ✓ Mdalasini mzima vijiti vikubwa vitano ✓ Binzari nyembamba kibakuli kidogo kimoja ✓Karafuu kibakuli kidogo kimoja ✓ Pilipili manga kibakuli kidogo kimoja ✓ Hiliki nzima kibakuli kidogo kimoja ✓ Uwatu kibakuli kidogo kimoja ✓Mustard seed kibakuli kidogo kimoja MATAYARISHO 1. Chukua frying pan weka jikoni weka na viungo vyako vyote Kisha koroga kidogo kidogo ili usiviunguze (Moto uwe wa kiasi visiungue) 2. Ukimaliza ipua na viache vipoe 3. Chukua blender ya kusagia viungo na uvisage Kisha vitakuwa tayari kutumiwa (Kama hauna blender chukua kinu kidogo na mchi na uviponde ponde Kisha chekecha kwa kichujio Cha chai, japo itakuchukua mda kidogo) Kama umependezwa na pishi langu la leo weka comment hapo chini au Kama unaswal

JINSI YA KUPIKA NDIZI MASALA.

Image
NAFASI ZA SENSA 2022 www.tamisemi.go.tz JIANDAE KUHESABIWA Karibu tena katika darasa letu la mapishi mbalimbali ukiwa na mimi International Admin. Basi leo tupo na pishi la ndizi mshale za masala. Enjoy! MAHITAJI ✓ Ndizi mshale . ✓ Binzari ya njano ( Turmeric powder) ✓Nyama ✓ Karoti ✓Njegere ✓ Vitunguu maji ✓ Tangawizi ✓ Kitunguu swaum ✓ Mafuta kiasi ✓ Nazi ✓ Curry Powder MATAYARISHO. 1. Chemsha nyama ikishaiva menya ndizi mshale osha na uziweke. 2. Weka binzari ya njano (Turmeric powder) kijiko kimoja Cha chai weka na chumvi kiasi 3. Weka curry powder kijiko kimoja Cha chakula. 4. Chukua tangawizi na kitunguu swaum vilivyosagwa weka 4. Weka kitunguu maji, njegere na Karoti Kisha koroga taratibu usivunje ndizi acha mpaka ndizi na njegere ziive. 5. Weka tui zito la nazi koroga kidogokidogo mpaka liive (Kama chumvi utaona imepungua unaweza kuongeza kidogo) 6. Ndizi zako zitakuwa tayari kupakuliwa utakunywa na kinywaji chochote ukipen

MAPISHI YA KUKU SEKELA.

Image
NAFASI ZA SENSA 2022 www.tamisemi.go.tz JIANDAE KUHESABIWA Karibuni sana katika darasa letu zuri la mapishi. Leo tutaangalia namna ya kumtengeneza kuku mtamu wa sekela au wengine wanaita Tandoor Chicken MAHITAJI ✓ Kuku 1Kg.(mpasue kati) ✓Ukwaju 1/2pakti (katika kikombe kimoja Cha maji) ✓kitunguu Swaum (kijiko 1 Cha chakula) ✓Tangawizi (kijiko 1 Cha chakula ) ✓Binzari nyembamba ya unga (uzile) - kijiko 1 Cha chai. ✓Pilipili manga (kijiko 1 Cha chai) ✓Chumvi kiasi ✓Tandoori masala (kijiko 1 Cha chai) NAMNA. ✓ Safisha kuku vizuri Kisha wachuje maji (wengine wanapenda kutoa ngozi) ✓Loweka Ukwaju na maji kikombe kimoja Kisha koroga mpaka urojo uwe mzito Chuja Kama tui la nazi ondoa kokwa Kisha mimina kwenye kuku. ✓weka vitunguu swaum na tangawizi Kisha changanya ✓ weka pilipili manga, uzile na chumvi Kisha changanya vizuri. ✓weka tandoori masala Kisha changanya vizuri na uache Kama dakika 30 ivi viungo vikolee vizuri kisha mpake

JINSI YA KUTENGENEZA UBUYU WA BABU ISSA

Image
NAFASI ZA SENSA 2022 www.tamisemi.go.tz JIANDAE KUHESABIWA Kama ambavyo tunajua ubuyu huu ni pendwa Sana na watu hasa kwa wewe mjasiriamali ni vema ukajifunza. MAHITAJI 1. Sukari (vikombe 2 vya chai) 2. Maji (Vikombe vikubwa 2) 3. Ubuyu wa tunda (vikombe 4) 4. Ubuyu wa Unga (nusu kikombe) 5. Pilipili ya Unga (robo kijiko) 6. Chumvi ya Unga (Robo kijiko) 7. Hiliki ya Unga (robo kijiko ) 8. Rangi nyekundu au yoyote. NAMNA ✓ Chukua sifuria weka maji yachemke changanyana sukari, chumvi, pilipili ya Unga, rangi na hiliki ✓ Mimina ubuyu wa tunda na kuroga kwa dakika mbili ✓ Mimina ubuyu wa Unga na koroga ✓Baada ya hapo Mimina kwenye chombo Cha wazi na uache upoe Kama umependeza somo langu la leo weka comment hapo chini au Kama unaswali nitakujibu punde. KARIBU TENA

JINSI YA KUTENGENEZA TAMBI NZURI ZA DENGU

Image
NAFASI ZA SENSA 2022 www.tamisemi.go.tz JIANDAE KUHESABIWA Kwanza kabisa nikuhakikishie kuwa tambi za namna hii ni nzuri na tofauti kabisa na unazoziona barabarani. Kajaribu halafu utarudi kutoa mrejesho hasa kwa wajasiriamali hizi utaziuza Sana. MAHITAJI 1. Unga wa dengu (8-10)Kg 2. Sukari (2Kg) 3. Ngano (2Kg) 4. Manjano (kijiko 1) 5. Chicken Masala (Kijiko 1) 6. Kitunguu swaum kilichopondwa kiasi 7.Baking powder ya Simba ya blue (nusu kijiko) 8. Pilipili manga (Kijiko 1) 9. Chumvi kiasi 10. Maji ya vuguvugu (lita 3-4) 11. Mafuta ya kula NAMNA YA KUTENGENEZA ✓ Changanya mchanganyo wote kasoro maji mpaka vichanganyike ✓ Weka maji ya vugu vugu mpaka mchanganyo wako uwe laini Kama ugali wa mtoto ✓ Chota mchanganyo wako weka kwenye kifaa Cha kutengenezea tambi ✓ Hakikisha mafuta yamepata moto vizuri ✓ Kaanga tambi kwenye mafuta (Koroga Mara moja) ✓ Chuja mafuta kwenye tambi baada ya kuzitoa jikoni > ✓ Subiri zipoe na tambi zako zitak