Posts

Showing posts with the label Maisha

HISTORIA YA SAMIA SULUHU HASSAN

Image
Samia Suluhu Hassan alizaliwa mnamo tarehe 27/01/1960 katika visiwa vya Zanzibar. Alianza elimu ya msingi mnamo 1966-1972 katika shule tofauti tofauti zilizopo Unguja na Pemba yaani Zanzibar. Alianza katika shule ya CHAWAKA (Unguja), Kisha alihamia katika shule ya msingi ZIWANI (Pemba) na alimaliza katika shule ya msingi ya Mahonda. Elimu yake ya sekondari alianza 1973-1976 .Alisoma katika shule mbili, 1973-1975 alisoma katika shule ya sekondari ya Ngambo (Unguja) Kisha mwaka 1976 alihamia shule ya Lumumba (Unguja) ambapo alihitimu elimu ya sekondari. Hakuendelea tena na masomo ya chuo kwa muda huo. Aliajiriwa katika serikali ya Zanzibar Kama mchapishaji ambapo alipanda ngazi na kuwa Afisa mipango mnamo 1987-1988. Samia Suluhu Hassan alijiendeleza kielimu huku akiwa mtumishi wa serikali kwa kusoma kozi fupi mbalimbali Kama vile Sheti ya takwimu kabla ya kujiunga na Taasisi ya Maendeleo na uongozi ya Mzumbe Morogoro ambapo alifanikiwa kuhitimu stashahada ya juu ya utawala

PESA HUWA ZINAJIFICHA WAPI?

Image
NAFASI ZA SENSA 2022 www.tamisemi.go.tz JIANDAE KUHESABIWA Watu wengi siku hizi tunahangaika kutafuta pesa lakini hatujui pesa zimejificha wapi. Hapa nataka nikuoneshe sehemu tano ambazo pesa hujificha. 1.KIPAJI CHAKO Watu wengi wenye vipaji sasa hivi ndio wanaoingiza pesa ndefu Sana kwa urahisi ndani ya muda mchache na wanahitajika Kila siku. Chukulia mfano. Mkandarasi akatangaza uwepo wake ukumbini kiingilio Tsh.500/= watakuja watu wangapi? Wewe utakwenda? Lakini diamond platnumz akitangaza atakuwepo kwa kiingilio Cha shilingi elfu tatu maelfu ya watu watamiminika. Watu wengi sasa hivi wanalipwa kwa kuhudumia watu wengi mfano Mbwana Samatta akiingia uwanjani maelfu na Malaki ya watu hufurahi hivyo basi anapata pesa nyingi kutokana na watu wengi na kupata balozi mbalimbali. Lakini daktari atahudumia wagonjwa tu waambao kwa siku huenda akahudumia sio zaidi ya mia moja.Hivyo basi hata Kama una taaluma yako lakini bado unatakiwa ukijue kipaji chak

NAMNA YA KUWEKA BAJETI

50% ya kipato chako iweke kwa ajili ya matumizi yako ya Kila siku Kama chakula, mavazi, umeme, Kodi, maji n.k Watu wengi huwa wanajipunja Sana hapa na ndo mana unaishi kwa kujitesa. Kama unaingiza 1M basi laki tano itenge kwa ajili ya hayo mahitaji muhimu ya mara kwa mara Kama vile chakula, umeme, Kodi, nauli na mavazi. Watu wengi wakipata fedha wanaweka akiba yote na kusahau kuwa Kuna vitu wanavihitaji kila siku, si ajabu kukuta mtu ameweka akiba na bado amekopa madeni mengi tu kwa ajili ya chakula. Hapa utawasikikia watu mimi siwezi kuweka akiba bwana , kila nikiweka naila! wanasahau kwamba hutakiwi kuweka pesa yote unayoipata kama akiba kwa sababu itakushinda tu, utahitaji kula utaanza kula akiba. Tunatafuta pesa ili tujikimu kimaisha na sio kujitesa kimaisha. Lakini kumbuka kuweka nusu tu ya kipato chako kwenye mahitaji muhimu 30% ya kipato chako itenge kwa ajili ya matakwa yako (your wants) mfano: unataka kununua gari, unataka kutoka out, unataka kumfanyia mtu surp

MAMBO YA KUYAACHA ILI UFANIKIWE

1.KUACHA KUSIKILIZA WATU WANAOKUKATISHA TAMAA Watu wakukukatisha tamaa hawawezi kukosekana yawezekana ni familia yako, ndugu zako, mpenzi wako, rafiki yako, walimu wako, wafanyakazi mwenzako, jirani zako Kama anakukatisha tamaa usimsikilize Kuna watu wao Kila siku wapo kukatisha watu tamaa tu na kama ikitokea umeanguka kidogo utasikia si unaona nilisema Mimi hukuniskiliza, Mimi najua... basi hapo kwake furaha tele akiona na wewe kweli umekata tamaa. 2.KUACHA KUJILAUMU KWA MAKOSA YA NYUMA Kuna watu kwa sababu tu alishafanya kosa fulani katika maisha yake basi ndo atajihukumu hadi anaingia kaburini, Mimi nilifanya iki jamani labda ndo sababu n.k hata mungu husamehe na kupotezea makosa. Wewe sio mkosaji Kama Farao hupaswi kujilaumu kwa makosa uliyofanya yakakupelekea kufeli. 3.KUACHA KUJIDHARAU Ukijidharau wewe mwenyewe nani atakaekuamini? Hayupo jikubali na usijishushe. Jiamini katika unachokifanya wewe sio wakuwa chini siku zote. 4.KUKAA KWA MUDA MREFU BILA KUFANYA MAAMUZI K

SEHEMU 9 ZITAKAZOKUFANYA UWE MILLIONAIRE

Image
International Admin 1. HUDUMA ZA KIFEDHA (financial services) Hapa unaweza kufanya huduma mbalimbali Kama vile za kibenki, uwakala wa mitandao ya simu na bank, mikopo,makampuni ya bima n.k watu wengi hujipatia fedha kupitia mifumo hiyo Kama uwakala hakikisha unalenga eneo linalokuwa na mjongeo wa watu wengi Kama vile barabarani, vyuoni,n.k Unaweza kwenda kufungua bonus account kwa NMB bank kima Cha chini ni elfu hamsini yani hizo bonus account wewe unakuwa unaiacha pesa yako kwa miezi kuanzia 3 bila kuitoa ila wanakuwa wanakulipa kwa ongezeko la asilimia fulani kwa mwezi kadri unavoiacha. Kwa hiyo utalipwa kutokana na kiwango Cha pesa zako wanakuwa na % za kugawa faida. Au unaweza kununua hisa (shares) kwa wale wasioelewa hisa naomba niwatolee mfano: Mimi na marafiki zangu 3 tunaanzisha kampuni mtaji ulotumika elfu kumi, mimi nimetoa elfu 5 mmoja katoa elfu 3 na mwingine elfu mbili kwahiyo mgawanyo wetu wa umiliki wa ile kampuni Mimi nitamiliki 50% mwingine ata

LIFE STAR

Image
International Admin Maisha ni Kama nyota unayoiona juu angani ili ufurahie maisha inabidi uwe na pembe tano Kama nyota. Utaweza kuyafurahia maisha yako kwa amani na raha kama utazingatia pembe tano zifuatazo za maisha yako. 1. MUNGU Haimaanishi Sasa uanze kukesha msikitini/kanisani ndo utakuwa karibu na mungu bali mshirikishe mungu katika chochote unachofanya maana hata mchawi humuomba mungu "eh mwenyezi mungu nijaalie nifanikiwe kumroga fulani" mda mwingine mambo yetu hayaendi kwa sababu hatumtegemei mwenyezi mungu. Kama mwenyezi mungu anasaidia waja wake wa aina zote wachamungu, washirikina, wahalifu. Iweje ashindwe kukusaidia pale utakapo muomba? Tumtegemee mwenyezi mungu kwa kila kitu tunachokifanya. 2. PESA Utashindwa kufanya chochote unachokitaka kukifanya kama hauna pesa, badala yake utaishia kutamani tu " dah! natamani ningekuwa na hela ningesaidia familia yangu, ningesaidia masikini, ningefanya...n.k." (hauwezi kutoa

SABABU ZITAKAZO FANYA UCHELEWE KUFIKA KATIKA MAFANIKIO

KUPENDA RAHA Kuna watu hawapedi kujitesa wanapenda raha sana kula bata sana wanasahau Kama wanatakiwa kupamba wawe na uchumi mzuri. Kwa hali hii utakesha ukitafuta mafanikio KUGHAIRISHA MAMBO. Kila Jambo analolipanga anaghairisha unasema utaanza kesho utaanza kuwa serious kesho utafanya hiki badae. Unaamka unasema utafanya hiki leo unajikuta hujafanya unahamishia kesho hivo hivo mpaka Leo una viporo vya mambo mengi ambayo haukuyafanya bado. MIPANGO MINGI BILA HATUA. Kuna watu wakichukua notebook zao na madaftari wakaanza kukusimulia mipango yao yani utavutiwa na kusema safi sana lakini hakuna hatua yoyote wanayoichukua kuyafanyia kazi mawazo yao. Hivyo basi usiwe mtu wa namna hii mipango mingi Matendo machache. KUSOMA BILA KUELIMIKA. Kuna watu wamesoma lakini wanashindwa kutumia elimu yao kuiishi katika maisha yao. Wewe umeenda kujifunza kutengeneza kitu fulani lakini utabaki tu kusimulia nilienda kufundishwa kutengeneza cake Mimi na hautaki