VIGEZO VYA KULIPWA YOUTUBE

Karibu sana katika blog yangu Leo naenda kukuletea vigezo vya kulipwa YouTube. Kwanza kabisa mtu yeyote anaweza kumiliki account ya YOUTUBE na akalipwa. Kitendo Cha wewe kuwa na account ya email ya Google (Gmail) tayari inakufanya uwe na YouTube account. YouTube ni mtandao ambao unazidi kushika Kasi na kuingizia kipato watu wengi kila siku. Una uwezo wa kuweka videos zako watu wakaangalia na ukalipwa pia.
VITU VYA KUWA NAVYO WAKATI WA KUFUNGUA ACCOUNT YA YOUTUBE
1. Fungua Gmail account katika simu yako.
JINSI YA KUFUNGUA GMAIL ACCOUNT
✓ Ingia Google
✓ Andika Gmail sign up
✓ Utaletewa form ya kujaza taarifa zako binafsi
✓ Kisha utakubaliana na masharti ya Gmail kwa kubonyeza kitufe kilichoandikwa Agree baada ya kujaza form yako
✓ Tayari utakuwa na Google account (Gmail)
2. Baada ya kuwa na account ya Google utaingia youtube uta click kwenye icon ya juu kabisa upande wa kulia itakayokuwa inawakilisha Gmail account yako.
3. Utaenda katika my channel
4. Utaenda sehemu yenye alama ya setting
5. Kisha uta edit taarifa zako kadiri ya upendavyo.
6. Mpaka hapo tayari una YouTube account yako
JINSI YA KUPOST YOUTUBE
✓ Ingia katika file la video katika simu yako
✓ Ichague video unayoitaka kui post YouTube
✓ Bonyeza kwenye Share ( zitatokea application nyingi YouTube, Instagram, Facebook, WhatsApp, n.k) utachagua icon ya YouTube
✓ Itakuleta sehemu ambayo utaandika kichwa Cha habari Cha video yako na maelezo
✓ Kisha utabonyeza kwenye POST na video yako itaruka YouTube.
ZINGATIA
✓Chagua jina la channel litakalokuwa rahisi kukumbukwa na lisiwe refu mfano tbc, ITV, wasafi,bona, Ayo, n.k
✓Chagua jina lenye kuvutia ✓Usitumie jina la channel nyingine
✓Usichukue video yenye hati miliki ya mtu mwingine ukaituma YouTube, hii itafanya ufungiwe au usilipwe.

VIGEZO VYA KULIPWA YOUTUBE
Lazima ujiunge na Google AdSense
Google AdSense ni kampuni ya matangazo ambayo inatumika kuwalipa watu kwenye forum, apps, YouTube, blogs na website mbalimbali kwa njia ya matangazo. Baada ya kujiunga na Google AdSense na kufikisha vigezo utaanza kupokea matangazo. Kwa hiyo utalipwa kutokana na matangazo, Kama mnavoonaga ukiingia YouTube channel nyingi yanaanza matangazo halafu video inafata. Ukishaanza kulipwa utapokea hela (USD)kwa mfumo wa PayPal, pioneer, Western Union au njia zingine za kupokelea pesa. AdSense itakulipa kutokana na idadi ya watakaotazama tangazo la kwenye video yako (impression) mfano:
Watu 1000 --- 0.5$-1$ USD
Watu 100,000 ---100$ USD
VIGEZO VYA KUJIUNGA NA GOOGLE ADSENSE
1. Uwe na masaa elfu 4000 ( watch time hours)
Huu ni jumla ya muda ambao watu wameitazama video katika channel yako ya YouTube. Ni vema ukawa na video ndefu kiasi kuanzia dakika tano ili kumfanya mtu aangalie channel yako na uweze kufikisha masaa 4000 kwa urahisi. Lakini pia isiwe ndefu Sana kwani itamfanya mtu asiangalie yote akaboeka au akapeleka mbele na hapo utahesabika muda ambao tu ameutumia hata Kama alirusha video. Ndo mana siku hizi watu wanatafuta vichwa vya habari vitakavomfanya mtazamaji aangalie mwanzo mwisho. Mfano: TIZAMA JINSI MTOTO MCHANGA ANAVYOZUNGUMZA kila mtu atataka kuona mtoto mdogo ataongeaje lakini mwisho wa video hajaongea unabaki kukasirika lakini mwenzako ushamuongezea masaa. Sisemi watu ndo waanze kufanya hivi ila waandae vitu vitakavyowafanya watu wavutiwe kuendelea kuangalia.
2.Uwe na wafuasi 1000 (subscriber) Unatakiwa uwakumbushe waku ku subscribe katika channel yako katika kila video Kama ukipenda.
3. Channel yako iwe na watazamaji (viewers) kuanzia elfu kumi 10,000
4. Uwe ume verify channel yako kwa njia ya simu.
5. Uwe katika nchi zinazokubalika kupokea malipo ya YouTube Tanzania ni miongoni pia. NB: Kama unataka kupata pesa nzuri zaidi ni vema ukawa na maudhui yatakayogusa nchi nyingi kwani watazamaji wa nchi zingine wakiwa wengi pesa inapatikana nzuri pia. Kama wewe ni mchekeshaji basi fanya comedy zako dunia nzima au sehem nyingi wakuangalie ili upate hela ya maana


Kama upependezwa na umejifunza kitu kutokana na post yangu hii ya leo. Weka Comment hapo chini πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

KARIBU TENA

Comments

Popular posts from this blog

VITU VYA KUFANYA KARIBIA NA MITIHANI.

CHEKA WITH INTERNATIONAL ADMIN

JINSI YA KUANDAA VIUNGO VYA PILAU VYENYE HARUFU NZURI.